MKUU wa wilaya ya Chunya ambaye ni Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbeya,Mrakibu Mwandamizi wa jeshi la uhamiaji,Alhaji Mubarak Batenga amewataka wazazi na walezi waliopatiwa msaada wa vitimwendo kwa ajili ya watoto wenye ulemavu kuvitumia kuwapeleka shule badala ya kuendelea kukaa nao ndani ili elimu wanayopata iwe na manufaa katika maisha yako ya badae.









