![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2024/02/6000-1024x682.png)
Na Esther Macha, Timesmajira, Online, Mbeya
Wananchi 6,000, mkoani Mbeya wamewezeshwa bima za afya bure na taasisi ya Tulia Trust kupitia Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Dkt.Tulia Ackson ikiwa ni jitihada za kuunga mkono serikali katika sekta ya afya.
Akiwakabidhi bima hizo wananchi hao leo
Naibu Waziri Mkuu,Waziri wa Nishati Dkt.Doto Biteko,amesema kuwa kitendo kilichofanywa na Dkt.Tulia kutoa bima za afya bure kwa wananchi mkoani Mbeya ni jambo la ibada ambalo lengo ni kupata huduma bora za afya na kusema kwamba hilo ni somo kwa walio wengi hususani Wabunge waliochaguliwa.
Sanjari na hayo Dkt.Biteko amesema kwamba licha ya Dkt.Tulia kuwakilisha wananchi wa Mbeya Bungeni lakini bado anawakilisha nchi duniani hivyo imani yake kubwa kwa watu wa Mbeya watailinda heshima yake.
“Sisi Wabunge wenzako na tuliopo serikalini utakapokuwa unasimamia shughuli za Bunge tutahakikisha kila linalowezekana kuondoa changamoto zote zilizopo katika Jimbo hili tunaziondoa kabisa kwani itakuwa ajabu sana umepata heshima ya kidunia bado uendelee kuhangaika na changamoto ndogo ndogo za zahanati,”amesema Dkt.Biteko.
Kwa upande wake Spika wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini ambaye pia ni Rais umoja wa Mabunge Duniani, Dkt.Tulia Ackson amesema kuwa bima za afya ambazo zinatolewa kwa wananchi pamoja na kwamba hawana vyama wanaenda kupata huduma ambako CCM imefanya kazi nzuri.
Dkt. Tulia amesema kuwa, bima hizo zinazotolewa na Taasisi ya Tulia zitawawezesha wananchi kupata matibabu hadi ngazi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.
Taasisi ya Tulia imekuwa na utaratibu wa kutoa bima hizo za afya kwa Wazee, Watu wenye ulemavu na kaya zenye uhitaji ambapo kutoka mwaka 2019 hadi sasa jumla ya kaya 2670 zimefaidika huku idadi ya wananchi wakiwa ni 16,020 na zoezi hilo linaendelea.
“Kuhusu hospitali ya wazazi Meta mnajua namna ilivyokuwa huko nyuma sasa hivi huduma zimekuwa bora zimeingia zaidi ya bilioni 17 .3 jengo limekamilika,wanasubiri Rais Samia aje kunzindua rasmi maana tayari kumeboreshwa vizuri,”amesema Dkt.Tulia.
Chifu Mkuu wa mkoa wa Mbeya Rocket Mwashinga,ameomba kuwe na dirisha la wazee kwani wanapata shida pindi wanapofika kupata huduma za matibabu katika hospitali na vituo vya afya pamoja na zahanati na kuomba wazee na watoto waheshimiwe na kuthaminiwa .
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…
April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]