TULIA TRUST KUGUSA WALEMAVU KUPITIA MPANGO WA UWEZESHAJI KIUCHUMI

Taasisi ya Tulia Trust imeanza programu maalum ugawaji wa baiskeli za viti mwendo kwa walemavu sambamba na kuwaingiza kwenye mpango wa kuwezesha kiuchumi.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kubaini kundi kubwa la walemavu kuishi maisha ya tabu kwa kukosa usaidizi ikiwepo miradi ya kujipatia kipato cha kujikimu.

Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema leo Jumanne Machi 12, 2024 wakati akikabidhi kitimwendo kwa mlemavu Zaina Mbwalo (50) mkazi wa mtaa wa  Kabwina Kata ya Sinde jijini hapa.

“Kupitia Mlemavu Zainabu tumebaini kuna mahitaji makubwa watakatiwa mitaji ili kuanzisha miradi ya kiuchumi”.

Mwakanolo amesema kama Taasisi waliweka malengo yao ni kutoa viti mwendo kwa walemavu kata 36 lakini baada ya kuanza zoezi imebainika wahitaji ni wengi.

Pia Taasisi hiyo imeweza kutoka madaftari katika Shule za Hasanga na Kilimo Bonge la Uyole ambapo pia imeelezwa mahitaji bado ni makubwa huku malengo yalikuwa kutoka kwa watoto 3,000 wenye mahitaji kutoka kaya zisizojiwe.

 

“Mahitaji ya Walengwa yamekuwa makubwa tofauti  na tulivyitarajia lakini tutawafikia wahitaji wote wakiwepo walemavu na watoto wenye mazingira magumu mashuleni” amesema.

 

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa kiti mwendo, Mlemavu Zaina amesema kuwa kwa kipindi cha miaka 30 ameishi kwa tabu licha ya kujihusisha na biashara ndogo ndogo.

“Nikitaka kutoka kufuata mahitaji nalazimika kuita vijana wanibebe na kulipa gharama kulingana na umbali huku akitoa mfano, kwenda kanisani ni Sh 4,000” amesema.

Amesema anamshukuru kwa msaada huo huku akieleza kuhitaji  kiasi cha Sh 1 milioni ili kuagiza udongo wa kutengenezea majiko” amesema.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

DONATE

Give us a call or fill in the form below and we'll contact you. We endeavor to answer all inquiries within 24 hours on business days. DONATE BY BANK: Account Name: TULIA TRUST Account Number: 0150226766000 Bank Name: CRDB