“Miaka ya nyuma wagonjwa waliokuwa wakipewa rufaa walikuwa wakisafirishwa lakini sasa huduma zote zinapatikana katika hosptali yetu ya Kanda na bado tunaendelea kupokea fedha kwa ajili ya kuendeleza huduma ikiwepo za wagonjwa wa dharura sambamba na vituo vya afya na zahanati” amesema.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, ameagiza Wizara ya afya, Hosptali, vituo vya afya na zahanati kuboresha na kuyasimamia madirisha ya wazee nchini.
Amewataka watoa huduma wasiwavunje Moyo wazee wanapofika kupatiwa huduma kwa kutambua kuwa ndio wamelifikisha taifa hapa lililo kwa ushirikiano na mshikamano.
Katika hatua nyingine amesema kama wabunge kitendo alichokifanya Dkt. Tulia kimewapa darasa kwa kutoa bima za afya kwa kaya 1,000 zenye watu 6,000.
Naye, Waziri wa Maji Jumaa Aweso amechangia Sh 10 milioni kwa ajili ya kuendeleza mpango wa utoaji za bima za afya kwa wananchi wa jimbo la Mbeya kupitia Taasisi ya Mbunge wa Mbeya mjini, Spika wa Bunge na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU).
Amesema kitendo anachofanya Dkt. Tulia anawapa somo kwani amekuwa ni Mbunge anayejua anafanya nini licha ya kuwa kiongozi mkubwa kwenye dunia lakini kila akija ziara Mkoa wa Mbeya lazima anamkuta na anaeleza matatizo ya wananchi wake.
Kwa upande wake Mratibu wa zoezi la ugawaji wa bima za afya, Frank Kalinga amesema kwa kipindi cha miaka mitano wametoa bima za afya kwa kaya 2,670 zenye wahitaji 16,020 katika Mkoa wa Mbeya.
Amesema bado mahitaji ni makubwa na kumuomba Mkurugenzi wa Taasisi hiyo kuona namna katika awamu nyingine kuzifikia kaya nyingine zenye uhitaji.
Mnufaika wa mpango huo, Fredy Pondo ameshukuru Taasisi ya Tulia Trust kwani imeweza kuthamini maisha ya wananchi wa kipato cha chini kuwapatia bima za afya zitakazo wasaidia kupata huduma za afya bure.
Recent Posts
- Vegas Hero Casino: Zijn d…March 11, 2026Vegas Hero Casino, een dynamische speler in de online gokindustrie, heeft de aandacht getrokken van […]
- True Luck Casino offre-t-…March 7, 2026En tant qu’analyste en ligne spécialisé dans les casinos depuis plusieurs années, j’ai examiné avec […]
- Der Froggybet Kosmos: Ein…March 6, 2026Als SEO-Kopiräfter mit zehn Jahren Erfahrung im iGaming-Bereich habe ich viele Online-Casinos […]
- Lizaro Casino: een diepga…March 6, 2026Het lizaro online casino heeft zichzelf gepositioneerd als een aantrekkelijke optie voor online […]
- De gebruikersinterface va…March 6, 2026Million Casino is een interessante nieuwkomer in de online gokwereld, die zich richt op zowel […]






