![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2024/02/6000v-1024x682.png)
“Miaka ya nyuma wagonjwa waliokuwa wakipewa rufaa walikuwa wakisafirishwa lakini sasa huduma zote zinapatikana katika hosptali yetu ya Kanda na bado tunaendelea kupokea fedha kwa ajili ya kuendeleza huduma ikiwepo za wagonjwa wa dharura sambamba na vituo vya afya na zahanati” amesema.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, ameagiza Wizara ya afya, Hosptali, vituo vya afya na zahanati kuboresha na kuyasimamia madirisha ya wazee nchini.
Amewataka watoa huduma wasiwavunje Moyo wazee wanapofika kupatiwa huduma kwa kutambua kuwa ndio wamelifikisha taifa hapa lililo kwa ushirikiano na mshikamano.
Katika hatua nyingine amesema kama wabunge kitendo alichokifanya Dkt. Tulia kimewapa darasa kwa kutoa bima za afya kwa kaya 1,000 zenye watu 6,000.
Naye, Waziri wa Maji Jumaa Aweso amechangia Sh 10 milioni kwa ajili ya kuendeleza mpango wa utoaji za bima za afya kwa wananchi wa jimbo la Mbeya kupitia Taasisi ya Mbunge wa Mbeya mjini, Spika wa Bunge na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU).
Amesema kitendo anachofanya Dkt. Tulia anawapa somo kwani amekuwa ni Mbunge anayejua anafanya nini licha ya kuwa kiongozi mkubwa kwenye dunia lakini kila akija ziara Mkoa wa Mbeya lazima anamkuta na anaeleza matatizo ya wananchi wake.
Kwa upande wake Mratibu wa zoezi la ugawaji wa bima za afya, Frank Kalinga amesema kwa kipindi cha miaka mitano wametoa bima za afya kwa kaya 2,670 zenye wahitaji 16,020 katika Mkoa wa Mbeya.
Amesema bado mahitaji ni makubwa na kumuomba Mkurugenzi wa Taasisi hiyo kuona namna katika awamu nyingine kuzifikia kaya nyingine zenye uhitaji.
Mnufaika wa mpango huo, Fredy Pondo ameshukuru Taasisi ya Tulia Trust kwani imeweza kuthamini maisha ya wananchi wa kipato cha chini kuwapatia bima za afya zitakazo wasaidia kupata huduma za afya bure.
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…
April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]