TULIA TRUST YAWAPA TABASAMU WANA-ITEZI

TULIA TRUST YAWAPA TABASAMU WANA-ITEZI

Taasisi ya Tulia Trust imetoa Msaada wa Viti Mwendo Vinne (4) kwa Watu Wenye Uhitaji Maalumu (Watu wenye Ulemavu) kata ya Itezi Jijini Mbeya.

Zoezi hilo la kukabidhi viti mwendo limefanyika katika Uwanja wa Gombe likiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Mhe.Mubarak Alhaji Batenga akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini Mhe. Beno Malisa.

Katika zoezi hilo Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Mkurugenzi Wake ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson pia imekabidhi Daftari kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi Wanye uhitaji Kutoka mitaa minne ya Kata hiyo ya Itezi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

DONATE

Give us a call or fill in the form below and we'll contact you. We endeavor to answer all inquiries within 24 hours on business days. DONATE BY BANK: Account Name: TULIA TRUST Account Number: 0150226766000 Bank Name: CRDB