![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2024/03/WhatsApp-Image-2024-03-18-at-22.03.54_0f84f4fa-1024x576.jpg)
Na Esther Macha, TimesmajiraOnline,Mbeya
MKUU wa wilaya ya Chunya ambaye ni Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbeya,Mrakibu Mwandamizi wa jeshi la uhamiaji,Alhaji Mubarak Batenga amewataka wazazi na walezi waliopatiwa msaada wa vitimwendo kwa ajili ya watoto wenye ulemavu kuvitumia kuwapeleka shule badala ya kuendelea kukaa nao ndani ili elimu wanayopata iwe na manufaa katika maisha yako ya badae.
Viti mwendo hivyo vimetolewa na Taasisi ya Tulia Trust kwa wanafunzi wenye ulemavu na watu wazima ili viwe sehemu ya usaidizi badala ya kutegemea ndugu pekee ambao tayari wanakuwa na majukumu mengine ya kufanya.
Alhaji Batenga amesema hayo wakati akikabidhi vitimwendo vinne na madaftari kwa wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu katika kata ya Itezi Jijini Mbeya.
Amesema Tulia Trust imeshasaidia zaidi ya wanafunzi 3000 na vitimwendo 46 na kuomba waliopatiwa msaada kuvitumia vizuri kwa manufaa.
Akielezea zaidi Alhaji Batenga amesema kuwa kwa kitendo cha wenye ulemavu kupatiwa viti mwendo itapunguza idadi ya watu kupungua kumsindikiza mtu pale anapohitaji kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwasababu mtu mmoja anakwenda na watu wawili mpaka watatu na anayesindikiza shughuli za uzalishaji zinasimama pia inasamsaidia kwanza anahitaji kitimwendo hivyo uwepo wa kitimwendo utamsaidia mzazi kufanya shughuli za kiuchumi.
Joshua Mwakanolo ni Ofisa habari na mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust amesema kuwa mpaka sasa wamefikia kata 36 na Mitaa 181 ya Jiji la Mbeya ambapo lengo lilikuwa ni kutimiza ahadi ya mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust Dkt.Tulia Ackson kuweza kuwasaidia madaftari wanafunzi wenye uhitaji na watu wenye ulemavu 46 na wanafunzi 3000 na kwa kata ya Itezi wamekabidhi viti mwendo vinne.
Kwa upande wake Katibu wa siasa na uenezi chama cha mapinduzi kata ya Itezi , Raphael Mwaitege amewataka wanasiasa kuacha kubeza misaada inayotolewa na Dkt.Tulia.
“Unakuta mtu ni mnufaika jioni anakaa kumsema vibaya Dkt.Tulia kuwa hana kazi yeyote huyo mtu lazima apimwe akili,ndugu zangu wananchi tushindane kwa vitendo na Tulia akileta baiskeli za watu wenye ulemavu wewe leta bajaji wakati mwingine mwanasiasa akilemaa na siasa anaweza akawa kichaa”amesema Mwaitege.
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…
April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]