![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2024/04/IMG-20240411-WA0011-1024x682.jpg)
Sheikh wa Mkoa wa Mkoa Mbeya, Msafiri Njalambaha amesema kitendo anachokifanya Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani na Spika wa Bunge Dkt. Tulia kuigusa jamii ni sadaka na kutekeleza maagizo ya Mungu visihusishwe na masuala ya kisiasa.
Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.
Amesema Dkt. Tulia amekuwa msaada mkubwa kwa dini ya kiislam kwani licha ya kuwafutulisha pia amekuwa akichangia ujenzi wa misikiti, jamii yenye mahitaji.
“Tunaona mchango wake mkubwa, sio sasa ni zaidi ya miaka mitatu anatoa futari kwa waumini wenye hali duni na hivi karibuni tumepokea mchele kilo 400 tende katoni 20 hii ni sadaka isihusishwe na masuala ya kisiasa” amesema.
Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) Mkoa wa Mbeya, Ndele Mwaselela amesema CCM imetulia na Dkt. Tulia na kwamba watamlinda na kuhakikisha uchaguzi Mkuu 2025 anapitia kwa kishindo.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera amemtaja Dkt. Tulia ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya mjini kuwa ni kiongozi wa kuigwa na mfano amekuwa chachu ya kuleta maendeleo katika Jimbo la Mbeya na Mkoa kwa ujumla.
“Tunayaona anayofanya ameweza kujenga nyumba saba kwa wahitaji, kutoa sare za shule kwa watoto 3,000 kujenga misikiti na hata jitihada zake kuleta miradi mikubwa ikiwoeo barabaraa njia nne na stendi kubwa ya kisasa ya mabasi ya Mikoa, kama CCM tutamlindaa hao wengine waachane na siasa wakafanye biashara”.
Mwenyeki wa CCM, Mkoa Patrick Mwalunenge ameunga mkono kauli ya viongozi hao na kwamba watamlinda Dkt. Tulia Ackson kuendelea na majukumu ya Bunge wao wanachama kazi jimboni.
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]DKT. TULIA KUMSAIDIA MATI…
April 11, 2024Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson ametoa ahadi ya kumpatia matibabu ya mguu Mzee mwenye mahitaji Mbaliki Shikunzi(80).[…]