Wazee wasiojiweza Jijini Mbeya wameanza kutabasamu baada ya Taasisi ya Tulia Trust kuanza program ya kugawa chakula na mavazi bure.
Programu hiyo imeanza leo katika baadhi ya Kata lengo ni kuhakikisha wahitaji wanafikiwa huku kikosi kazi cha Taasisi ya Tulia Trust kikiendesha zoezi hilo kulingana na idadi ya waliobainika.
Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi hiyo, Joshua Mwakanolo amesema lengo ni kuhakikisha wazee wasiojiweza wanatabasamu kwa kupata mahitaji muhimu.
“Mpango huu ni kutekeleza maono ya Mkurugenzi wetu ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge, na Mbunge wa Jimbo la Mbeya, Dkt. Tulia Ackson” amesema.
Amesema bado wanaenda kuhakikisha jamii inatabasamu ikiwepo ujenzi wa makazi bora kutoa viti mwendo kwa watu wenye walemavu.
Mkazi wa Jijini Mbeya, Lazaro Juma ameishukuru Taasisi hiyo akiwepo Mkurugenzi wake Dkt. Tulia Ackson kwa kugusa wazee waliosahaulika katika jamii na kuonekana ni wasumbufu.
“Ni mtu wa kipekee sana kwa kipindi kifupi amegusa jamii ya wenye mahitaji wakiwepo watoto wenye mazingira magumu kupata sare za shule, madaftari na hata ujenzi wa makazi bora kwa wahitaji jambo ambalo lina thawabu kubwa mbele za Mungu” amesema.
Recent Posts
- WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]
- DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]
- SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]
- MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]
- VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]