Wazee wasiojiweza Jijini Mbeya wameanza kutabasamu baada ya Taasisi ya Tulia Trust kuanza program ya kugawa chakula na mavazi bure.
Programu hiyo imeanza leo katika baadhi ya Kata lengo ni kuhakikisha wahitaji wanafikiwa huku kikosi kazi cha Taasisi ya Tulia Trust kikiendesha zoezi hilo kulingana na idadi ya waliobainika.
Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi hiyo, Joshua Mwakanolo amesema lengo ni kuhakikisha wazee wasiojiweza wanatabasamu kwa kupata mahitaji muhimu.
“Mpango huu ni kutekeleza maono ya Mkurugenzi wetu ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge, na Mbunge wa Jimbo la Mbeya, Dkt. Tulia Ackson” amesema.
Amesema bado wanaenda kuhakikisha jamii inatabasamu ikiwepo ujenzi wa makazi bora kutoa viti mwendo kwa watu wenye walemavu.
Mkazi wa Jijini Mbeya, Lazaro Juma ameishukuru Taasisi hiyo akiwepo Mkurugenzi wake Dkt. Tulia Ackson kwa kugusa wazee waliosahaulika katika jamii na kuonekana ni wasumbufu.
“Ni mtu wa kipekee sana kwa kipindi kifupi amegusa jamii ya wenye mahitaji wakiwepo watoto wenye mazingira magumu kupata sare za shule, madaftari na hata ujenzi wa makazi bora kwa wahitaji jambo ambalo lina thawabu kubwa mbele za Mungu” amesema.
Recent Posts
- 1win Apostas E Casino Aqu…May 3, 20241win Apostas E Casino Aqui No Brasil ᐈ Registro Electronic Login Ao Site Oficial Da 1win” […]
- Zakłady Bukmacherskie Par…May 3, 2024Zakłady Bukmacherskie Parimatch Bonusy, Recenzja I Skargi Online Betting Best Sports Betting […]
- 2024 RevieMay 3, 20242024 Review Raging Bull Casino ️ Honest Online Online Casino Review 【2020】 Content Table Games At […]
- 1xbet Venezuela Empresa D…May 3, 20241xbet Venezuela Empresa De Apuestas ᐉ Apuestas Deportivas En Línea Sign In 1xbet ᐉ Empieza 1xbet […]
- Glory Casino Online In Ba…May 2, 2024Glory Casino Online In Bangladesh Online Gambling Venue Inside Bangladesh Content Customer Support […]