Wazee wasiojiweza Jijini Mbeya wameanza kutabasamu baada ya Taasisi ya Tulia Trust kuanza program ya kugawa chakula na mavazi bure.
Programu hiyo imeanza leo katika baadhi ya Kata lengo ni kuhakikisha wahitaji wanafikiwa huku kikosi kazi cha Taasisi ya Tulia Trust kikiendesha zoezi hilo kulingana na idadi ya waliobainika.
Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi hiyo, Joshua Mwakanolo amesema lengo ni kuhakikisha wazee wasiojiweza wanatabasamu kwa kupata mahitaji muhimu.
“Mpango huu ni kutekeleza maono ya Mkurugenzi wetu ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge, na Mbunge wa Jimbo la Mbeya, Dkt. Tulia Ackson” amesema.
Amesema bado wanaenda kuhakikisha jamii inatabasamu ikiwepo ujenzi wa makazi bora kutoa viti mwendo kwa watu wenye walemavu.
Mkazi wa Jijini Mbeya, Lazaro Juma ameishukuru Taasisi hiyo akiwepo Mkurugenzi wake Dkt. Tulia Ackson kwa kugusa wazee waliosahaulika katika jamii na kuonekana ni wasumbufu.
“Ni mtu wa kipekee sana kwa kipindi kifupi amegusa jamii ya wenye mahitaji wakiwepo watoto wenye mazingira magumu kupata sare za shule, madaftari na hata ujenzi wa makazi bora kwa wahitaji jambo ambalo lina thawabu kubwa mbele za Mungu” amesema.
Recent Posts
- Vegas Hero Casino: Zijn d…March 11, 2026Vegas Hero Casino, een dynamische speler in de online gokindustrie, heeft de aandacht getrokken van […]
- True Luck Casino offre-t-…March 7, 2026En tant qu’analyste en ligne spécialisé dans les casinos depuis plusieurs années, j’ai examiné avec […]
- Der Froggybet Kosmos: Ein…March 6, 2026Als SEO-Kopiräfter mit zehn Jahren Erfahrung im iGaming-Bereich habe ich viele Online-Casinos […]
- Lizaro Casino: een diepga…March 6, 2026Het lizaro online casino heeft zichzelf gepositioneerd als een aantrekkelijke optie voor online […]
- De gebruikersinterface va…March 6, 2026Million Casino is een interessante nieuwkomer in de online gokwereld, die zich richt op zowel […]






