![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2024/04/IMG-20240404-WA0024-1024x682.jpg)
Taasisi ya Tulia Trust imetoka kilo 400 za mchele na tende boksi 20 katika Msikiti Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa ajili ya waumini wenye mahitaji katika kuelekea sikuu ya Eid El Fitri.
Ofisa habari na mawasilino wa Taasisi ya Tulia Trust Joshua Mwakanolo amekabidhi mahitaji hayo kwa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Msafiri Njalambaha katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya msikiti wa Mkoa barabara ya Saba jijini hapa.
Akizungumza kwa niaba ya Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson, Mwakanolo amesema lengo ni kuona wahitaji wanasherekea sikuu ya Eid El Fitri kama jamii nyingine.
“Nimesimama kwa niaba ya Mkurugenzi wa nimekabidhi mchele kilo 400 na tende boksi 20 kikubwa ni kuona wenzetu wanasherekea kwa furaha kama jamii nyingine” amesema.
Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Msafiri Njalambaha amesema kitendo kinachofanywa na Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini na Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson mbali na masuala ya kisiasa amekuwa akijitolea kusaidia watu wenye uhitaji kama ibada kipindi cha mwezi mtukufu .
“Nimepokea futari kwa niaba ya waislamu ni kitu kinaonyesha mtu anajitoa kwa ajili ya Mungu wake watu wasimchukulue kama anafanya kwa masuala ya kiasiasa” amesema
Naye Imani msikiti wa Baraa Bin Azb Isanga,Shekhe Ibrahim Bombo wataendelea kumuombea Dkt. Tulia kwani amekuwa kiungo kikubwa katika kuisaidia jamii.
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…
April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]