Muktasari:
- Amesema viongozi waliopo sasa, akiwamo Rais Samia Suluhu Hassan, wana matarajio na dhamira ya kuendelea kuhudumia wananchi, hivyo kuimba wimbo huo kwa sasa kungeweza kuonekana kama ishara ya kutotamani kuendelea na majukumu yao.
Mwanga. Wakati Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson akieleza namna alivyoshindwa kuimba wimbo wa “Moyo wangu una furaha ya kwenda mbinguni” katika ibada ya mazishi ya hayati Cleopa Msuya, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, alitumia jukwaa hilo kumkumbuka tukio la mwaka 1990, Msuya alipowasaidia yeye na waziri wake usafiri wa kurudi ofisini, baada ya baraza la mawaziri kuvunjwa wakajikuta hawana usafiri.
Ibada hiyo ya mazishi ilifanyika katika Usharika wa Usangi Kivindu, wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakuu wa kitaifa.
Dk Tulia alieleza kuwa hakuweza kuimba wimbo huo kwa sababu ujumbe wake ulihusu utayari wa kwenda mbinguni, jambo ambalo alilihusianisha moja kwa moja na hali ya kisiasa, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
“Niliamua kukaa kimya na kusikiliza kwa makini. Nikasema, nashukuru askofu alituruhusu tusio tayari tusiimbe. Sisi tunaotazamia uchaguzi 2025 hatujaimba, si kwa sababu hatutaki kwenda mbinguni, bali tunaomba kwenda baadaye,” alisema Dk Tulia kwa ucheshi uliopokelewa kwa vicheko na tafakari.
Dk Tulia amesema aliathiriwa sana na ujumbe wa wimbo huo ambao ulizungumzia utayari wa kwenda mbinguni. Wimbo huo namba 157, fungu la tatu, kutoka katika kitabu cha ‘Tumwabudu Mungu wetu uliombwa kuimbwa na Mkuu wa
Kanisa hilo, Askofu Dk Alex Malasusa.
Hata hivyo, Dk Tulia amesema hakushiriki kuimba wimbo huo na alimshukuru Askofu Malasusa kwa kuelewa na kuruhusu wale ambao hawakuwa tayari, kutouimba.
“Kuna neno unasikia na unajua linakuhusu. Kila mmoja amechukua kile kinachomgusa, lakini mimi nilikaa kimya, nikasikiliza kwa makini sana ule wimbo unaosema ‘mbinguni tunao utayari’. Nikaona siwezi kuimba, kwa sababu sina utayari wa kwenda sasa,” alisema Dk Tulia.
“Nashukuru kwa kuturuhusu tusio tayari tusiimbe… Sasa hivi tuna mtazamo na matarajio, tuna Rais wetu Samia Suluhu Hassan ambaye tunamtarajia, na sisi wengine wenye matarajio pia, hatukuimba.”
Recent Posts
- Vegas Hero Casino: Zijn d…March 11, 2026Vegas Hero Casino, een dynamische speler in de online gokindustrie, heeft de aandacht getrokken van […]
- True Luck Casino offre-t-…March 7, 2026En tant qu’analyste en ligne spécialisé dans les casinos depuis plusieurs années, j’ai examiné avec […]
- Der Froggybet Kosmos: Ein…March 6, 2026Als SEO-Kopiräfter mit zehn Jahren Erfahrung im iGaming-Bereich habe ich viele Online-Casinos […]
- Lizaro Casino: een diepga…March 6, 2026Het lizaro online casino heeft zichzelf gepositioneerd als een aantrekkelijke optie voor online […]
- De gebruikersinterface va…March 6, 2026Million Casino is een interessante nieuwkomer in de online gokwereld, die zich richt op zowel […]






