![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2024/01/WhatsApp-Image-2024-01-27-at-11.35.38_b7f393d7-723x1024.jpg)
Taasisi inawakaribisha Watanzania wote kwenye mashindano ya riadha yajulikanayo kama MBEYA TULIA MARATHON msimu wa Nane mashindano yatafanyika mnamo tarehe 10-11/05/2024 uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya kuanzia saa 12:00 asubuhi.
Ijumaa ya tarehe 10/05/2024 yatafanyika mashindano ya mbio fupi yaani M100, M200, M400, M800 na 1500M, ambapo siku ya Jumamosi tarehe 11/05/2024 yatafanyika mashindano ya mbio ndefu yaani KM5, KM10, KM21 na KM42 ikiwa ni pamoja na kukabidhi zawadi kwa washindi wote wa riadha kwa siku zote mbili.Pamoja na hayo tutakua na vituo kadhaa vya kuuzia namba za usajili ili uweze kushiriki kikamilifu kuwania ushindi wa MBEYA TULIA MARATHON 2024, Vifuatavyo ni vituo utakavyoweza kujisajili kushiriki Mbeya Tulia Marathon;
MKOA WA MBEYA.
- Tukuyu – Ofisi ya Tulia Trust +255 753 176328
- Uyole – Ofisi ya Tulia trust +255 755 682187
- Kyela – Ofisi ya Tulia Trust +255 769 737637
- Kabwe – Friendship Stationery +255 769 846832
- Mwanjelwa – Nasra House of Fashion +255 767 454772
- Mwanjelwa – Light Shop +255 769 300702
MKOA WA ARUSHA
Sheikh Amri Abeid Stadium +255 769 846832
Tunawakaribisha Wajasiriamali wote kutumia fursa hiyo ya kufanya biashara zao bila gharama yeyote, pamoja na hayo kutakua na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa kizazi kipya pamoja na burudani za ki asili (ngoma za jadi), Maelezo zaidi piga simu namba +255 763 828271.
JOSHUA EDWARD
AFISA HABARI NA MAWASILIANO TULIA TRUST
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…
April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]