DKT. TULIA APEWA TANO KUWEZESHA WANANCHI

Na Esther Macha , Timesmajira Online, Mbeya

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Spika wa Bunge,Dkt Tulia Ackson,Novemba 12,2024,amewakabidhi nyumba wahitaji watatu wanaoishi katika mazingira magumu Kata za Iyunga mtaa wa Inyala na kata ya Ilemi jijini humo.

Ambapo katika kumuunga mkono Dkt.Tulia Wabunge wa Jimbo la Mbarali Bahati Ndingo na Mbunge wa Jimbo la Rungwe,Mwantona walikabidhi kiasi cha shilingi 600,000 kwa wahitaji hao.

Huku Mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya Bahati Ndingo,amesema Dkt.Tulia, amewezesha kiuchumi wananchi wa Jimbo hilo wakiwemo vijana,wanawake na wazee.Ambapo ni kiongozi wa mfano anayepaswa kuheshimiwa na kulindwa.

“Hakuna kundi ambalo Dkt.Tulia ameliacha katika uwezeshaji wananchi kiuchumi,ikiwemo kuwezesha vijana pikipiki 100, na wengine kiuchumi,wazee bima za afya, wanawake wamewezeshwa mikopo ili waweze kufanya shughuli za uzalishaji.Hata kwangu Mbarali ameweza kusaidia ingawa siyo Jimbo lake,”amesema.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Rungwe,Antony Mwantona amesema kwa umoja wao wataendelea kumuunga mkono Dkt.Tulia kwani licha ya kusaidia makundi mbalimbali jijini hapa,bado amekuwa akisaidia hata wananchi wasiokuwa wa Jimbo la Mbeya Mjini hivyo anapaswa kulindwa kwa nguvu zote.

Soma Zaidi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

DONATE

Give us a call or fill in the form below and we'll contact you. We endeavor to answer all inquiries within 24 hours on business days. DONATE BY BANK: Account Name: TULIA TRUST Account Number: 0150226766000 Bank Name: CRDB