Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson amekabidhi mahitaji ukiwemo mchele tani mbili kwa wazee 3,000 wanaoishi mazingira magumu katika kata 36 na mitaa 181 Jijini Mbeya.
Dkt. Tulia amekabidhi mahitaji hayo, Desemba 20, 2024 na kuweka bayana lengo ni kuhakikisha wazee wanaungana na watanzania kusherehekea sikukuu ya Krismas.
Amesema lengo lingine la msaada huo ni kuwapa tabasamu wazee na watu wenye ulemavu kuhakikisha wanaungana na watanzania wengine kusherekea sikukuu hiyo.
“Watanzania tujenge utamaduni wa kuwashika mkono wazee ili watabasamu kwa kutambua furaha uongeza siku za kuishi,”amesema.
Dkt. Tulia amefafanua kuwa awamu hii walengwa ni wale wenye hali duni ambao hawajiwezi na kubainisha katika awamu nyingine watayagusa makundi mengi.
“Naomba msijikie vibaya ambao hampo kwenye orodha kwani tulitoa maelekezo kwa viongozi wenu kwa walengwa tulio wahitaji ambao wamepewa mchele kilo 2 na kiasi cha Sh. 5,000″ameongeza.
Kapwile Kapwile ambaye ni mnufaika wa msaada huo, amemshukuru Dkt. Tulia na kueleza kwamba ni Mbunge wa kwanza Jimbo la Mbeya mjini kukumbuka kundi la watu wenye uhitaji.
Recent Posts
- Vegas Hero Casino: Zijn d…March 11, 2026Vegas Hero Casino, een dynamische speler in de online gokindustrie, heeft de aandacht getrokken van […]
- True Luck Casino offre-t-…March 7, 2026En tant qu’analyste en ligne spécialisé dans les casinos depuis plusieurs années, j’ai examiné avec […]
- Der Froggybet Kosmos: Ein…March 6, 2026Als SEO-Kopiräfter mit zehn Jahren Erfahrung im iGaming-Bereich habe ich viele Online-Casinos […]
- Lizaro Casino: een diepga…March 6, 2026Het lizaro online casino heeft zichzelf gepositioneerd als een aantrekkelijke optie voor online […]
- De gebruikersinterface va…March 6, 2026Million Casino is een interessante nieuwkomer in de online gokwereld, die zich richt op zowel […]






