TULIA TRUST YAGUSA WALEMAVU, WAZEE MAHITAJI YA CHAKULA NA KUBORESHA MAKAZI.
![](https://tuliatrust.org/wp-content/uploads/2023/12/IMG-20231225-WA0031-1024x682.jpg)
Taasisi ya Tulia Trust imekabidhi mahitaji ya chakula kwa wahitaji Wilayani Rungwe kwaajili ya Sikukuu ya Krismasi. Msaada huo uliokabidhiwa kwa kaya 13 ni pamoja na mchele, maharage na mafuta ya kula vyenye jumla ya thamani ya Sh. milioni 3.
“Wahitaji hao walibainika kupitia mbio za bendera hiyo kutoka Tulia Trust zilizofanyika wilayani Rungwe zilizobeba Ujumbe wa kuhamasisha Upendo, Uwajibikaji na Mshikamano” amesema Mwakanolo.
Amesema mpango huo wa taasisi umetolewa kupitia program ya Tulia Trust Mtaani Kwetu ambayo inalenga kuwasaidia watu wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Mwakanolo amesema mbali na misaada huo wa chakula pia wameanza ujenzi na ukarabati wa makazi ya walemavu na wazee wanaoishi kwenye makazi hatarishi.
“Kuna nyumba za mahitaji wiwili tumeanza ujenzi baada ya kubaini makazi yao sio salama na kuwa katika hatari na haya ni maelekezo ya Mkurugenzi wa taasisi Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) katika kuisaidia jamii” amesema Mwakanolo.
Mwakanolo amesema lengo la taasisi hiyo ni kuona jamii hususani wazee na walemavu wanakuwa sehemu salama kama jamii nyingine ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali kuondoa changamoto kwa watanzania wenye mahitaji.
Kwa upande wake kikongwe Never Kisuru (80) amemshukuru Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson kwa moyo wa kujitolea kwa wenye mahitaji pasipo kujali itikadi vya vyama wala udini.
“Maisha yangu nilikuwa naishi kwenye nyumba ya mianzi lakini leo hii taasisi hii baada ya kunitembelea nimeanza kujengwa makazi bora ambayo yataniwezesha kuwa salama” amesema Kisuru.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2023/12/tulia-trust-yagusa-walemavu-wazee.html
Recent Posts
WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]SPIKA DKT. TULIA AMJENGEA…
April 11, 2024Akiongea huku akibubujikwa machozi Singwava Jackson amemshukuru Dkt Tulia kwa kuisitiri familia yake kwani alikuwa akiishi kwenye turubai kwa hofu hasa mvua zilipokuwa zikinyesha na pia hakuwa na mtaji.[…]MNEC MWASELELA: MBEYA TUM…
April 11, 2024Mwaselela amesema hayo Aprili 8, mwaka huu wakati akitoa salamu kwenye Iftar iliyoandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake mbaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson jijini hapa.[…]VIONGOZI MBEYA WASEMA DKT…
April 11, 2024Sheikh Njalambaha amesema usiku wa jana Aprili 8 mwaka huu wakati wa waumini wa dini ya kiislam, viongozi wa Chama, Serikali na Machifu mkoani hapa walipoungana kula aftari iliyoandaliwa, Dkt. Tulia Ackson kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.[…]