TULIA TRUST YAGUSA WALEMAVU, WAZEE MAHITAJI YA CHAKULA NA KUBORESHA MAKAZI.

Taasisi ya Tulia Trust imekabidhi mahitaji ya chakula kwa wahitaji Wilayani Rungwe kwaajili ya Sikukuu ya Krismasi. Msaada huo uliokabidhiwa kwa kaya 13 ni pamoja na mchele, maharage na mafuta ya kula vyenye jumla ya thamani ya Sh. milioni 3.
“Wahitaji hao walibainika kupitia mbio za bendera hiyo kutoka Tulia Trust zilizofanyika wilayani Rungwe zilizobeba Ujumbe wa kuhamasisha Upendo, Uwajibikaji na Mshikamano” amesema Mwakanolo.
Amesema mpango huo wa taasisi umetolewa kupitia program ya Tulia Trust Mtaani Kwetu ambayo inalenga kuwasaidia watu wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Mwakanolo amesema mbali na misaada huo wa chakula pia wameanza ujenzi na ukarabati wa makazi ya walemavu na wazee wanaoishi kwenye makazi hatarishi.
“Kuna nyumba za mahitaji wiwili tumeanza ujenzi baada ya kubaini makazi yao sio salama na kuwa katika hatari na haya ni maelekezo ya Mkurugenzi wa taasisi Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) katika kuisaidia jamii” amesema Mwakanolo.
Mwakanolo amesema lengo la taasisi hiyo ni kuona jamii hususani wazee na walemavu wanakuwa sehemu salama kama jamii nyingine ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali kuondoa changamoto kwa watanzania wenye mahitaji.
Kwa upande wake kikongwe Never Kisuru (80) amemshukuru Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson kwa moyo wa kujitolea kwa wenye mahitaji pasipo kujali itikadi vya vyama wala udini.
“Maisha yangu nilikuwa naishi kwenye nyumba ya mianzi lakini leo hii taasisi hii baada ya kunitembelea nimeanza kujengwa makazi bora ambayo yataniwezesha kuwa salama” amesema Kisuru.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2023/12/tulia-trust-yagusa-walemavu-wazee.html
Recent Posts
DKT. TULIA AHAMASISHA MAM…
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DKT.TULIA AMEREJESHA FURA…
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]BENJA FC WABABE WA TULIA …
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DKT. TULIA ASISITIZA MATU…
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]WANAFUNZI WAMTAJA DKT. TU…
August 21, 2024Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]