
Taasisi ya Tulia Trust leo imefanya matukio mawili likiwepo la kukabidhiwa madaftari kwa watoto wenye mahitaji maalum 3,000 katika shule la za msingi kata 36 jijini hapa.
Akikabidhi msaada wa kitimwindo, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema kuwa bado wataendelea kutoa viti mwendo kwa walemavu wenye uhitaji katika kata zote 36 za Jiji la Mbeya.
“Leo tumekuja kutoa misaada ya madaftari kwa wanafunzi 3,000 ambao walipata ya sare za shule za msingi kupitia Mkurugenzi wa Taasisi na Spika wa Bunge, Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya mjini ,Dk Tulia Ackson
Mwakanolo amesema kama Taasisi bado wataendelea kushirikiana na familia ya Doreen kuhakikisha anapata msaada mbalimbali sambamba na mzazi wake kuingizwa kwenye mpango wa kuwezesha wajasirimali ili atunishe miradi wake na kuweza kumhudumia.
Akizungumza mara baada ya kupata msaada wa kitimwindo, Doreen ambaye alishindwa kujizuia na kububujikwa. machozi amesema anamshukuru kwa msaada huo.
“Nilikuwa nikichelewa kufika shuleni wakati mwingine nikifika nakuta wenzangu wameanza masomo naomba serikali inisaidie nikimaliza elimu ya msingi nipete shule maalum” amesema.
Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule hiyo Ezekiel amesema kwa mwaka huu anatarajia kuhitimu elimu ya msingi wanaomba serikali kumtengenezea mazingira mazuri katika kuelekeza elimu ya Sekondari.
“Ni Mwanafunzi anayefanya vizuri kwenye masomo hivyo ili kutimiza malengo yake atengenezewe mazingira mazuri katika elimu ya Sekondari ikiwepo shule maalum za walemavu na sio za kata” amesema.
Mbali na msaada huo pia imemgusa Mwanafunzi mlemavu wa miguu Doreen Myuki (12) anayesoma darasa la saba katika shule ya Msingi Mwasote Jijini hapa aliyekuwa akibebwa kwa miaka saba mgongoni akipelekwa shule na kurudi.
Recent Posts
NYOTA YA PILTON MUSA YAZI…
July 18, 2025Tulia Trust tunatoa pongezi nyingi sana kwa Aliyekuwa Mshindi wa Kwanza kwenye Mashindano ya Kusaka Vipaji yaliyo anzishwa na Rais wa[…]WANANCHI UYOLE WAMCHUKULI…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DKT.TULIA ATANGAZA KUGOMB…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]TULIA ASHINDWA KUIMBA WIM…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DK BITEKO: MARATHONI NI F…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]