
Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson amekabidhi mahitaji ukiwemo mchele tani mbili kwa wazee 3,000 wanaoishi mazingira magumu katika kata 36 na mitaa 181 Jijini Mbeya.
Dkt. Tulia amekabidhi mahitaji hayo, Desemba 20, 2024 na kuweka bayana lengo ni kuhakikisha wazee wanaungana na watanzania kusherehekea sikukuu ya Krismas.
Amesema lengo lingine la msaada huo ni kuwapa tabasamu wazee na watu wenye ulemavu kuhakikisha wanaungana na watanzania wengine kusherekea sikukuu hiyo.
“Watanzania tujenge utamaduni wa kuwashika mkono wazee ili watabasamu kwa kutambua furaha uongeza siku za kuishi,”amesema.
Dkt. Tulia amefafanua kuwa awamu hii walengwa ni wale wenye hali duni ambao hawajiwezi na kubainisha katika awamu nyingine watayagusa makundi mengi.
“Naomba msijikie vibaya ambao hampo kwenye orodha kwani tulitoa maelekezo kwa viongozi wenu kwa walengwa tulio wahitaji ambao wamepewa mchele kilo 2 na kiasi cha Sh. 5,000″ameongeza.
Kapwile Kapwile ambaye ni mnufaika wa msaada huo, amemshukuru Dkt. Tulia na kueleza kwamba ni Mbunge wa kwanza Jimbo la Mbeya mjini kukumbuka kundi la watu wenye uhitaji.
Recent Posts
NYOTA YA PILTON MUSA YAZI…
July 18, 2025Tulia Trust tunatoa pongezi nyingi sana kwa Aliyekuwa Mshindi wa Kwanza kwenye Mashindano ya Kusaka Vipaji yaliyo anzishwa na Rais wa[…]WANANCHI UYOLE WAMCHUKULI…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DKT.TULIA ATANGAZA KUGOMB…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]TULIA ASHINDWA KUIMBA WIM…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DK BITEKO: MARATHONI NI F…
July 18, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]