SHEIKH NJALAMBAHA AONYA FIKRA MBAYA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Muktasari:

Kauli hiyo imetolewa na Shekhe wa Mkoa wa Mbeya , Shekhe Msafiri Njalambaha  leo Jumatano Machi 19, 2025 baada ya kupokea futari kwa wahitaji 200 wa dini ya Kiislamu iliyotolewa na Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson.

Mbeya. Viongozi wa dini ya Kiislamu Mkoa wa Mbeya wamefanya dua maalumu ya kuliombea Taifa na viongozi wa Serikali akiwepo Rais Samia Suluhu Hassan katika kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba 2025.
Mbali na dua hilo wakikemea baadhi ya Watanzania kujiepusha na fikra mbaya za kujihusisha uvunjifu wa amani
na badala yake kuombea utulivu na amani kwa maslai ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.
Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Msafiri Njalambaha ametoa kauli hiyo leo Jumatano Machi 19, 2025 baada ya kufanya dua maalumu na kupokea futari za wahitaji 200 iliyotolewa na Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson kupitia Taasisi ya Tulia Trust.

Njalambaha amesema huu ni mwaka wa uchaguzi kama viongozi wa dini wanalojukumu kubwa kuungana na waumini
na Watanzania kuombea amani, utulivu na kukemea vitendo “Taifa letu limepata tunu ya viongozi wa ngazi za juu
wanawake akiwepo Rais Samia Suluhu Hassan na Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya, Dk Tulia Ackson, hivyo niwaombe Watanzania tuzitunze hizi tunu na tusikubali kuzipoteza,” amesema.

Wakati huo huo,Shekhe Njalambaha amewataka wananchi kutohusisha misaada inayotolewa na Mbunge wa Mbeya
mjini, Dk Tulia Ackson na masuala ya kisiasa kutokana na kuelekea kipindi cha uchaguzi. “Hii siyo mara ya kwanza kiongozi huyo kugusa wahitaji kila mwaka anatoa mahitaji katika kipindi cha mfungo wa Idd El-Fitr, niombe tu waumini na Watanzania kuendelea kumuombea na kuliombea Taifa akiwamo Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema.

Amesema matendo yanayofanywa, Dk Tulia kuigusa jamii ya Kimungu na siyo mara ya kwanza kugusa wahitaji.
Kwa upande wake, Mjumbe wa Baraza la Masheikhe Mkoa, Sheikh Ibrahim Bombo ameishukuru Taasisi ya Tulia Trust kwa utaratibu wake wa kugusa walengwa huku akiwataka maimamu wa misikiti iliyoguswa kuhakikisha walengwa wanafikiwa. “Tuna kila sababu ya kushukuru kwa mahitaji ya walengwa 200 katika misikiti mbalimbali katika Jiji la Mbeya, jukumu letu ni kuendelea kufanya dua kumuombea,” amesema.

Mwakilishi wa Taasisi ya Tulia Trust, Athuman Kapuya ameshukuru ushirikiano wa viongozi wa dini na kuomba kuendelea kumuombea Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya Mjini, Dk Tulia Ackson.

Amesema wataendeleza ushirikiano unaogusa jamii yenye mahitaji katika mfungo na kuelekea Sikukuu ya Idd.
Mnufaika Stumahi Michuzi amesema wataendelea kufanya dua kumuombe Mbunge wa Mbeya, Dk Tulia, Mungu aendelee kumzidishia kutokana na namna anavyojitoa kugusa jamii yenye uhitaji.

Soma Zaidi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

DONATE

Give us a call or fill in the form below and we'll contact you. We endeavor to answer all inquiries within 24 hours on business days. DONATE BY BANK: Account Name: TULIA TRUST Account Number: 0150226766000 Bank Name: CRDB




    vulkan vegas, vulkan casino, vulkan vegas casino, vulkan vegas login, vulkan vegas deutschland, vulkan vegas bonus code, vulkan vegas promo code, vulkan vegas österreich, vulkan vegas erfahrung, vulkan vegas bonus code 50 freispiele, 1win, 1 win, 1win az, 1win giriş, 1win aviator, 1 win az, 1win azerbaycan, 1win yukle, pin up, pinup, pin up casino, pin-up, pinup az, pin-up casino giriş, pin-up casino, pin-up kazino, pin up azerbaycan, pin up az, mostbet, mostbet uz, mostbet skachat, mostbet apk, mostbet uz kirish, mostbet online, mostbet casino, mostbet o'ynash, mostbet uz online, most bet, mostbet, mostbet az, mostbet giriş, mostbet yukle, mostbet indir, mostbet aviator, mostbet casino, mostbet azerbaycan, mostbet yükle, mostbet qeydiyyat