Tulia Trust > News > Community Assistance > TULIA TRUST YAKABIDHI KITI MWENDO KWA MLEMAVU ALIYESOTA MIAKA SABA RUNGWE.
TULIA TRUST YAKABIDHI KITI MWENDO KWA MLEMAVU ALIYESOTA MIAKA SABA RUNGWE.

Taasisi ya Tulia Trust imekabidhi kiti mwendo kwa mtoto Ester Seme (7) mkazi wa kijiji cha Ilolo Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya alipata ulemavu tangu akiwa na umri wa mwaka mmoja mara baada ya kumpoteza mama yake mzazi.
Kiti hicho kimekabidhiwa jana na Ofisa Uhusiano na Mawasiliano, Joshua Mwakanolo kwa bibi wa mlemavu huyo Justina Seme (80) kwa lengo la kumsaidia kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Pia Mwakanolo alikabidhi bendera yenye ujumbe maalum wa uwajibikaji, upendo na ushirikishwaji kwa jamii ikiwa ni maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanganyika.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi kitimwendo, Mwakanolo amesema kitendo hicho ni kuikumbusha jamii kurejea kwenye dhana ya uwajibikaji, upendo, mshikamano na ushirikiano. Mwakanolo amesema umefika wakati sasa watanzania kuenzi utamaduni wetu kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya katika kusukuma mbele maendeleo ya watanzania. “Tutakuwepo kwa kipindi cha siku saba (wiki moja) kupeperusha bendera sambamba na kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii na elimu ya dhana nzima ya Uhuru wa Tanganyika” amesema.Akizungumza mara baada ya kupokea kitimwendo, Jestina Seme amesema analia machozi ya uzuni na furaha kwani hakikutarajia ipo siku mjukuu wake atakumbukwa na kupata matumaini ya kutoka nje na kujumuika na jamii nyingine” amesema. Amesema kuwa mama mzazi wa Ester alifariki mwaka 2016 alimuacha akiwa na mwaka mmoja na kuendelea kulea katika mazingira magumu kwani baba yake mzazi ajulikani alipo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Ilolo, Seti Bukuku amesema Dkt. Tulia Ackson amekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Rungwe licha ya kuwa Mbunge wa Mbeya mjini, Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Tanzania. “Wanarungwe tunaendelea kumuombea kwani ametugusa sana kwa msaada wa utoaji wa viti mwendo sana kwa mtoto, Ester familia yake ilikuwa katika kipindi kigumu cha kumsaidia miaka saba akiwa mlemavu” amesema.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2023/12/tulia-trust-yakabidhi-kiti-mwendo-kwa.html
Recent Posts
DKT. TULIA AHAMASISHA MAM…
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DKT.TULIA AMEREJESHA FURA…
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]BENJA FC WABABE WA TULIA …
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]DKT. TULIA ASISITIZA MATU…
May 30, 2025Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]WANAFUNZI WAMTAJA DKT. TU…
August 21, 2024Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]