
TAASISI isiyokuwa ya kiserikali ya Tulia Trust imeandaa mashindano ya Mbeya Tulia Marathon kwa msimu wa nane ambayo yanatarajiwa kuanza Mei 10 mpaka 11 mwaka huu lengo likiwa ni uboreshaji miundombinu ya elimu, afya pamoja na uwezeshaji kiuchumi kwa wananchi.
Hayo yamesemwa Januari 27,2024 na Ofisa Habari na Mawasiliano wa Tulia Trust, Joshua Edward wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya maandalizi ya mashindano ya Mbeya Tulia Marathon ambayo yatafanyika kuanzia Mei 10 mpaka 11 mwaka huu Jijini Mbeya katika uwanja wa Sokoine ambapo huu ni msimu wa nane toka yalipoanzishwa.
Edward amesema kuwa taasisi ya Tulia Trust kwa muda mrefu imekuwa ikijihusisha na uwezeshaji wananchi kiuchumi ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya elimu na afya.
“Yataanza kuanzia saa 12.00 asubuhi ambapo Mei 10 kutafanyika mbio fupi ambazo ni Mita 100,Mita 200,Mita 400,Mita 800, na Mita 1500 ambapo Mei 11 yatafanyika mashindano ya mbio ndefu ambazo ni Km 5,Km10,Km,21, pamoja Km 42 ikiwa ni pamoja na kukabidhi zawadi kwa washindi wote wa riadha kwa siku hizo mbili,”.
Pia amesema kuwa katika mashindano hayo kutakuwa na vituo kadhaa vya kuuzia namba za usajili ili uweze kushiriki kikamilifu katika kuwania ushindi huo wa Mbeya Tulia Marathon 2024.
“Katika haya mashindano tunakaribisha wajasiliamali mbali mbali kutumia fursa hii katika kufanya biashara zao bila gharama yeyote pamoj ili waweze kukuza vipato vyao “amesema.
Mratibu wa Tulia Trust Marathon ,Lwiza John amesema kuwa katika mashindano hayo suala la zawadi litakuwa pale pale kwa washiriki wa uwanjani na wa mbio za barabarani.
Joyce Mwakifwamba ni Ofisa Michezo Jiji la Mbeya amesema kuwa taasisi hiyo ni msaada mkubwa kwani imekuwa ikiangalia kila nyanja lakini bado katika eneo la michezo haijaacha kwenye ambapo kila mwaka wamekuwa wakikimbia ili kujenga afya zao.
“Ninaachoomba wakazi wa Mbeya tumuunge mkono Dkt.Tulia kwa sababu lengo lake ni nzuri ambalo ni kuimarisha miundombinu ya elimu na afya,”amesema Ofisa Michezo huyo.
https://timesmajira.co.tz/tulia-marathon-kurindima-mei-2024/
Recent Posts
WANAFUNZI WAMTAJA DKT. TU…
August 21, 2024Watoto watano waliokuwa wakiishi katika mazingira magumu waliopelekwa masomoni nchini Nigeria kwa ufadhili wa Taasisi ya Tulia Trust wamewasili nchini...[…]WALIOHITIMU ELIMU YA KIDA…
August 21, 2024Wanafunzi watano waliokuwa wakisoma nchini Nigeria kwa ufadhiri wa Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wa Spika wa Bunge Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) wamewasili leo Ijumaa Agost 16 mwaka huu.[…]1,000 KUSHIRIKI MASHINDAN…
August 21, 2024Mashindano hayo yanajulikana kama Tulia Cooking Festival yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi Agosti 2024 na yakishirikisha washiriki 1,000[…]WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO…
May 22, 2024Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 11, 2024 ameshiriki katika tukio la mbio za Mbeya Tulia Marathoni 2024[…]DKT. TULIA ATOA MSAADA KW…
April 22, 2024Dkt.Tulia Ackson amekabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa waathirika ambao nyumba zao zilifunikwa na maporomoko ya tope katika Mlimani Kawetele Kata ya Itezi jijini hapa na kusababisha kukosa makazi ya kuishi.[…]