TULIA ASHINDWA KUIMBA WIMBO WA MBINGU…

Muktasari:

  • Amesema viongozi waliopo sasa, akiwamo Rais Samia Suluhu Hassan, wana matarajio na dhamira ya kuendelea kuhudumia wananchi, hivyo kuimba wimbo huo kwa sasa kungeweza kuonekana kama ishara ya kutotamani kuendelea na majukumu yao.

Mwanga. Wakati Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson akieleza namna alivyoshindwa kuimba wimbo wa “Moyo wangu una furaha ya kwenda mbinguni” katika ibada ya mazishi ya hayati Cleopa Msuya, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, alitumia jukwaa hilo kumkumbuka tukio la mwaka 1990, Msuya alipowasaidia yeye na waziri wake usafiri wa kurudi ofisini, baada ya baraza la mawaziri kuvunjwa wakajikuta hawana usafiri.
Ibada hiyo ya mazishi ilifanyika katika Usharika wa Usangi Kivindu, wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakuu wa kitaifa.

Dk Tulia alieleza kuwa hakuweza kuimba wimbo huo kwa sababu ujumbe wake ulihusu utayari wa kwenda mbinguni, jambo ambalo alilihusianisha moja kwa moja na hali ya kisiasa, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

“Niliamua kukaa kimya na kusikiliza kwa makini. Nikasema, nashukuru askofu alituruhusu tusio tayari tusiimbe. Sisi tunaotazamia uchaguzi 2025 hatujaimba, si kwa sababu hatutaki kwenda mbinguni, bali tunaomba kwenda baadaye,” alisema Dk Tulia kwa ucheshi uliopokelewa kwa vicheko na tafakari.

Dk Tulia amesema aliathiriwa sana na ujumbe wa wimbo huo ambao ulizungumzia utayari wa kwenda mbinguni. Wimbo huo namba 157, fungu la tatu, kutoka katika kitabu cha ‘Tumwabudu Mungu wetu uliombwa kuimbwa na Mkuu wa
Kanisa hilo, Askofu Dk Alex Malasusa.

Hata hivyo, Dk Tulia amesema hakushiriki kuimba wimbo huo na alimshukuru Askofu Malasusa kwa kuelewa na kuruhusu wale ambao hawakuwa tayari, kutouimba.
“Kuna neno unasikia na unajua linakuhusu. Kila mmoja amechukua kile kinachomgusa, lakini mimi nilikaa kimya, nikasikiliza kwa makini sana ule wimbo unaosema ‘mbinguni tunao utayari’. Nikaona siwezi kuimba, kwa sababu sina utayari wa kwenda sasa,” alisema Dk Tulia.

“Nashukuru kwa kuturuhusu tusio tayari tusiimbe… Sasa hivi tuna mtazamo na matarajio, tuna Rais wetu Samia Suluhu Hassan ambaye tunamtarajia, na sisi wengine wenye matarajio pia, hatukuimba.”

Soma Zaidi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

DONATE

Give us a call or fill in the form below and we'll contact you. We endeavor to answer all inquiries within 24 hours on business days. DONATE BY BANK: Account Name: TULIA TRUST Account Number: 0150226766000 Bank Name: CRDB




    vulkan vegas, vulkan casino, vulkan vegas casino, vulkan vegas login, vulkan vegas deutschland, vulkan vegas bonus code, vulkan vegas promo code, vulkan vegas österreich, vulkan vegas erfahrung, vulkan vegas bonus code 50 freispiele, 1win, 1 win, 1win az, 1win giriş, 1win aviator, 1 win az, 1win azerbaycan, 1win yukle, pin up, pinup, pin up casino, pin-up, pinup az, pin-up casino giriş, pin-up casino, pin-up kazino, pin up azerbaycan, pin up az, mostbet, mostbet uz, mostbet skachat, mostbet apk, mostbet uz kirish, mostbet online, mostbet casino, mostbet o'ynash, mostbet uz online, most bet, mostbet, mostbet az, mostbet giriş, mostbet yukle, mostbet indir, mostbet aviator, mostbet casino, mostbet azerbaycan, mostbet yükle, mostbet qeydiyyat